• Sunrise At: 7:08 am
  • Sunset At: 5:03 pm
Go to Allah Before its to Late

Islamic: 23 Dhuʻl-Qiʻdah 1446 AH - Mon, Apr, 27, 2026

  • Fajr:3:25 am
  • Dhuhr:12:04 pm
  • Asr:5:00 pm
  • Maghrib:7:06 pm
  • Isha'a:8:45 pm
Sec Bottom Mockup

90: سورة البلد

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

In the Name of Allah—the Most Compassionate, Most Merciful.

Small toggle button
90:1
لَآ أُقْسِمُ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ ١

uq'simu bihādhā l-baladi


  Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.

Small toggle button
90:2
وَأَنتَ حِلٌّۢ بِهَـٰذَا ٱلْبَلَدِ ٢

wa-anta ḥillun bihādhā l-baladi


  Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.

Small toggle button
90:3
وَوَالِدٍۢ وَمَا وَلَدَ ٣

wawālidin wamā walada


  Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.

Small toggle button
90:4
لَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَـٰنَ فِى كَبَدٍ ٤

laqad khalaqnā l-insāna kabadin


  Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.

Small toggle button
90:5
أَيَحْسَبُ أَن لَّن يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌۭ ٥

ayaḥsabu an lan yaqdira ʿalayhi aḥadun


  Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?

Small toggle button
90:6
يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًۭا لُّبَدًا ٦

yaqūlu ahlaktu mālan lubadan


  Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»

Small toggle button
90:7
أَيَحْسَبُ أَن لَّمْ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ ٧

ayaḥsabu an lam yarahu aḥadun


  Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?

Small toggle button
90:8
أَلَمْ نَجْعَل لَّهُۥ عَيْنَيْنِ ٨

alam najʿal lahu ʿaynayni


  Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,

Small toggle button
90:9
وَلِسَانًۭا وَشَفَتَيْنِ ٩

walisānan washafatayni


  ulimi na midomo miwili ya kusemea

Small toggle button
90:10
وَهَدَيْنَـٰهُ ٱلنَّجْدَيْنِ ١٠

wahadaynāhu l-najdayni


  na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?

Small toggle button
90:11
فَلَا ٱقْتَحَمَ ٱلْعَقَبَةَ ١١

falā iq'taḥama l-ʿaqabata


  Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.

Small toggle button
90:12
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْعَقَبَةُ ١٢

wamā adrāka l-ʿaqabatu


  Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?

Small toggle button
90:13
فَكُّ رَقَبَةٍ ١٣

fakku raqabatin


  Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.

Small toggle button
90:14
أَوْ إِطْعَـٰمٌۭ فِى يَوْمٍۢ ذِى مَسْغَبَةٍۢ ١٤

aw iṭ'ʿāmun yawmin dhī masghabatin


  Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,

Small toggle button
90:15
يَتِيمًۭا ذَا مَقْرَبَةٍ ١٥

yatīman dhā maqrabatin


  yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,

Small toggle button
90:16
أَوْ مِسْكِينًۭا ذَا مَتْرَبَةٍۢ ١٦

aw mis'kīnan dhā matrabatin


  au masikini asiyekuwa na kitu.

Small toggle button
90:17
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْمَرْحَمَةِ ١٧

thumma kāna mina alladhīna āmanū watawāṣaw bil-ṣabri watawāṣaw bil-marḥamati


  Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.

Small toggle button
90:18
أُو۟لَـٰٓئِكَ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَيْمَنَةِ ١٨

ulāika aṣḥābu l-maymanati


  Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.

Small toggle button
90:19
وَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا هُمْ أَصْحَـٰبُ ٱلْمَشْـَٔمَةِ ١٩

wa-alladhīna kafarū biāyātinā hum aṣḥābu l-mashamati


  Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.

Small toggle button
90:20
عَلَيْهِمْ نَارٌۭ مُّؤْصَدَةٌۢ ٢٠

ʿalayhim nārun mu'ṣadatun


  Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.