Go to Allah Before its to Late
- Fajr:3:25 am
- Dhuhr:12:04 pm
- Asr:5:00 pm
- Maghrib:7:06 pm
- Isha'a:8:45 pm
73: سورة المزمل
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
In the Name of Allah—the Most Compassionate, Most Merciful.
yāayyuhā l-muzamilu
Ewe uliye jifunika!
qumi al-layla illā qalīlan
Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
niṣ'fahu awi unquṣ min'hu qalīlan
Nusu yake, au ipunguze kidogo.
aw zid ʿalayhi warattili l-qur'āna tartīlan
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
innā sanul'qī ʿalayka qawlan thaqīlan
Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.
inna nāshi-ata al-layli hiya ashaddu waṭan wa-aqwamu qīlan
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
inna laka fī l-nahāri sabḥan ṭawīlan
Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
wa-udh'kuri is'ma rabbika watabattal ilayhi tabtīlan
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
rabbu l-mashriqi wal-maghribi lā ilāha illā huwa fa-ittakhidh'hu wakīlan
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
wa-iṣ'bir ʿalā mā yaqūlūna wa-uh'jur'hum hajran jamīlan
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
wadharnī wal-mukadhibīna ulī l-naʿmati wamahhil'hum qalīlan
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
inna ladaynā ankālan wajaḥīman
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
waṭaʿāman dhā ghuṣṣatin waʿadhāban alīman
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
yawma tarjufu l-arḍu wal-jibālu wakānati l-jibālu kathīban mahīlan
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
innā arsalnā ilaykum rasūlan shāhidan ʿalaykum kamā arsalnā ilā fir'ʿawna rasūlan
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
faʿaṣā fir'ʿawnu l-rasūla fa-akhadhnāhu akhdhan wabīlan
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
fakayfa tattaqūna in kafartum yawman yajʿalu l-wil'dāna shīban
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
al-samāu munfaṭirun bihi kāna waʿduhu mafʿūlan
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
inna hādhihi tadhkiratun faman shāa ittakhadha ilā rabbihi sabīlan
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
inna rabbaka yaʿlamu annaka taqūmu adnā min thuluthayi al-layli waniṣ'fahu wathuluthahu waṭāifatun mina alladhīna maʿaka wal-lahu yuqaddiru al-layla wal-nahāra ʿalima an lan tuḥ'ṣūhu fatāba ʿalaykum fa-iq'raū mā tayassara mina l-qur'āni ʿalima an sayakūnu minkum marḍā waākharūna yaḍribūna fī l-arḍi yabtaghūna min faḍli l-lahi waākharūna yuqātilūna fī sabīli l-lahi fa-iq'raū mā tayassara min'hu wa-aqīmū l-ṣalata waātū l-zakata wa-aqriḍū l-laha qarḍan ḥasanan wamā tuqaddimū li-anfusikum min khayrin tajidūhu ʿinda l-lahi huwa khayran wa-aʿẓama ajran wa-is'taghfirū l-laha inna l-laha ghafūrun raḥīmun
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
QuranQari.Pk