Go to Allah Before its to Late
- Fajr:3:25 am
- Dhuhr:12:04 pm
- Asr:5:00 pm
- Maghrib:7:06 pm
- Isha'a:8:45 pm
15: سورة الحجر
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
In the Name of Allah—the Most Compassionate, Most Merciful.
alif-lam-ra til'ka āyātu l-kitābi waqur'ānin mubīnin
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
rubamā yawaddu alladhīna kafarū law kānū mus'limīna
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
dharhum yakulū wayatamattaʿū wayul'hihimu l-amalu fasawfa yaʿlamūna
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
wamā ahlaknā min qaryatin illā walahā kitābun maʿlūmun
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
mā tasbiqu min ummatin ajalahā wamā yastakhirūna
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
waqālū yāayyuhā alladhī nuzzila ʿalayhi l-dhik'ru innaka lamajnūnun
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
law mā tatīnā bil-malāikati in kunta mina l-ṣādiqīna
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
mā nunazzilu l-malāikata illā bil-ḥaqi wamā kānū idhan munẓarīna
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
innā naḥnu nazzalnā l-dhik'ra wa-innā lahu laḥāfiẓūna
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
walaqad arsalnā min qablika fī shiyaʿi l-awalīna
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
wamā yatīhim min rasūlin illā kānū bihi yastahziūna
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
kadhālika naslukuhu fī qulūbi l-muj'rimīna
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
lā yu'minūna bihi waqad khalat sunnatu l-awalīna
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
walaw fataḥnā ʿalayhim bāban mina l-samāi faẓallū fīhi yaʿrujūna
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
laqālū innamā sukkirat abṣārunā bal naḥnu qawmun masḥūrūna
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
walaqad jaʿalnā fī l-samāi burūjan wazayyannāhā lilnnāẓirīna
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
waḥafiẓ'nāhā min kulli shayṭānin rajīmin
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
illā mani is'taraqa l-samʿa fa-atbaʿahu shihābun mubīnun
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
wal-arḍa madadnāhā wa-alqaynā fīhā rawāsiya wa-anbatnā fīhā min kulli shayin mawzūnin
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
wajaʿalnā lakum fīhā maʿāyisha waman lastum lahu birāziqīna
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
wa-in min shayin illā ʿindanā khazāinuhu wamā nunazziluhu illā biqadarin maʿlūmin
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
wa-arsalnā l-riyāḥa lawāqiḥa fa-anzalnā mina l-samāi māan fa-asqaynākumūhu wamā antum lahu bikhāzinīna
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
wa-innā lanaḥnu nuḥ'yī wanumītu wanaḥnu l-wārithūna
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
walaqad ʿalim'nā l-mus'taqdimīna minkum walaqad ʿalim'nā l-mus'takhirīna
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
wa-inna rabbaka huwa yaḥshuruhum innahu ḥakīmun ʿalīmun
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
walaqad khalaqnā l-insāna min ṣalṣālin min ḥama-in masnūnin
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
wal-jāna khalaqnāhu min qablu min nāri l-samūmi
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
wa-idh qāla rabbuka lil'malāikati innī khāliqun basharan min ṣalṣālin min ḥama-in masnūnin
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
fa-idhā sawwaytuhu wanafakhtu fīhi min rūḥī faqaʿū lahu sājidīna
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
fasajada l-malāikatu kulluhum ajmaʿūna
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
illā ib'līsa abā an yakūna maʿa l-sājidīna
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
qāla yāib'līsu mā laka allā takūna maʿa l-sājidīna
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
qāla lam akun li-asjuda libasharin khalaqtahu min ṣalṣālin min ḥama-in masnūnin
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
qāla fa-ukh'ruj min'hā fa-innaka rajīmun
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
wa-inna ʿalayka l-laʿnata ilā yawmi l-dīni
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
qāla rabbi fa-anẓir'nī ilā yawmi yub'ʿathūna
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
qāla fa-innaka mina l-munẓarīna
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
ilā yawmi l-waqti l-maʿlūmi
Mpaka siku ya wakati maalumu.
qāla rabbi bimā aghwaytanī la-uzayyinanna lahum fī l-arḍi wala-ugh'wiyannahum ajmaʿīna
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
illā ʿibādaka min'humu l-mukh'laṣīna
Ila waja wako walio safika.
qāla hādhā ṣirāṭun ʿalayya mus'taqīmun
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
inna ʿibādī laysa laka ʿalayhim sul'ṭānun illā mani ittabaʿaka mina l-ghāwīna
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
wa-inna jahannama lamawʿiduhum ajmaʿīna
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
lahā sabʿatu abwābin likulli bābin min'hum juz'on maqsūmun
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
inna l-mutaqīna fī jannātin waʿuyūnin
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
ud'khulūhā bisalāmin āminīna
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
wanazaʿnā mā fī ṣudūrihim min ghillin ikh'wānan ʿalā sururin mutaqābilīna
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
lā yamassuhum fīhā naṣabun wamā hum min'hā bimukh'rajīna
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
nabbi ʿibādī annī anā l-ghafūru l-raḥīmu
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
wa-anna ʿadhābī huwa l-ʿadhābu l-alīmu
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
wanabbi'hum ʿan ḍayfi ib'rāhīma
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
idh dakhalū ʿalayhi faqālū salāman qāla innā minkum wajilūna
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
qālū lā tawjal innā nubashiruka bighulāmin ʿalīmin
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
qāla abashartumūnī ʿalā an massaniya l-kibaru fabima tubashirūna
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
qālū basharnāka bil-ḥaqi falā takun mina l-qāniṭīna
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
qāla waman yaqnaṭu min raḥmati rabbihi illā l-ḍālūna
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
qāla famā khaṭbukum ayyuhā l-mur'salūna
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
qālū innā ur'sil'nā ilā qawmin muj'rimīna
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
illā āla lūṭin innā lamunajjūhum ajmaʿīna
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
illā im'ra-atahu qaddarnā innahā lamina l-ghābirīna
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
falammā jāa āla lūṭin l-mur'salūna
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
qāla innakum qawmun munkarūna
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
qālū bal ji'nāka bimā kānū fīhi yamtarūna
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
wa-ataynāka bil-ḥaqi wa-innā laṣādiqūna
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
fa-asri bi-ahlika biqiṭ'ʿin mina al-layli wa-ittabiʿ adbārahum walā yaltafit minkum aḥadun wa-im'ḍū ḥaythu tu'marūna
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
waqaḍaynā ilayhi dhālika l-amra anna dābira hāulāi maqṭūʿun muṣ'biḥīna
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
wajāa ahlu l-madīnati yastabshirūna
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
qāla inna hāulāi ḍayfī falā tafḍaḥūni
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
wa-ittaqū l-laha walā tukh'zūni
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
qālū awalam nanhaka ʿani l-ʿālamīna
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
qāla hāulāi banātī in kuntum fāʿilīna
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
laʿamruka innahum lafī sakratihim yaʿmahūna
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
fa-akhadhathumu l-ṣayḥatu mush'riqīna
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
fajaʿalnā ʿāliyahā sāfilahā wa-amṭarnā ʿalayhim ḥijāratan min sijjīlin
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
inna fī dhālika laāyātin lil'mutawassimīna
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
wa-innahā labisabīlin muqīmin
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
inna fī dhālika laāyatan lil'mu'minīna
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
wa-in kāna aṣḥābu l-aykati laẓālimīna
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
fa-intaqamnā min'hum wa-innahumā labi-imāmin mubīnin
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
walaqad kadhaba aṣḥābu l-ḥij'ri l-mur'salīna
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
waātaynāhum āyātinā fakānū ʿanhā muʿ'riḍīna
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
wakānū yanḥitūna mina l-jibāli buyūtan āminīna
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
fa-akhadhathumu l-ṣayḥatu muṣ'biḥīna
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
famā aghnā ʿanhum mā kānū yaksibūna
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
wamā khalaqnā l-samāwāti wal-arḍa wamā baynahumā illā bil-ḥaqi wa-inna l-sāʿata laātiyatun fa-iṣ'faḥi l-ṣafḥa l-jamīla
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
inna rabbaka huwa l-khalāqu l-ʿalīmu
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
walaqad ātaynāka sabʿan mina l-mathānī wal-qur'āna l-ʿaẓīma
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
lā tamuddanna ʿaynayka ilā mā mattaʿnā bihi azwājan min'hum walā taḥzan ʿalayhim wa-ikh'fiḍ janāḥaka lil'mu'minīna
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
waqul innī anā l-nadhīru l-mubīnu
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
kamā anzalnā ʿalā l-muq'tasimīna
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
alladhīna jaʿalū l-qur'āna ʿiḍīna
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
fawarabbika lanasalannahum ajmaʿīna
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
ʿammā kānū yaʿmalūna
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
fa-iṣ'daʿ bimā tu'maru wa-aʿriḍ ʿani l-mush'rikīna
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
innā kafaynāka l-mus'tahziīna
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
alladhīna yajʿalūna maʿa l-lahi ilāhan ākhara fasawfa yaʿlamūna
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
walaqad naʿlamu annaka yaḍīqu ṣadruka bimā yaqūlūna
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
fasabbiḥ biḥamdi rabbika wakun mina l-sājidīna
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
wa-uʿ'bud rabbaka ḥattā yatiyaka l-yaqīnu
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
QuranQari.Pk